Soka Sports

je, bado hujawa member?

ni rahisi kuwa mwanajukwaa wa sokasports click register kutengeneza account yako.
itakuchukua sekunde 30 tu.

Join the forum, it's quick and easy

Soka Sports

je, bado hujawa member?

ni rahisi kuwa mwanajukwaa wa sokasports click register kutengeneza account yako.
itakuchukua sekunde 30 tu.

Soka Sports

Would you like to react to this message? Create an account in a few clicks or log in to continue.
Soka Sports

Jukwaa La Wanamichezo Tanzania www.sokasports.forumotion.com

FIFA WORLD CUP CHAMPONS 2018 FRANCE .

4 posters

    MZEE MAJUTO ANASEMA WEMA SEPETU AWEZI KUWA MKALI KUSHINDA RIHAMA JE NI KWELI?

    Dele Alli
    Dele Alli
    New Member
    New Member


    MZEE MAJUTO  ANASEMA WEMA SEPETU AWEZI KUWA MKALI KUSHINDA RIHAMA JE NI KWELI? Empty MZEE MAJUTO ANASEMA WEMA SEPETU AWEZI KUWA MKALI KUSHINDA RIHAMA JE NI KWELI?

    Post by Dele Alli Wed Apr 11, 2018 1:47 am

    Siku chache baada ya kufanyika kwa tuzo za Filamu zinazojulikana kama Sinema Zetu International Film Festival Award (SZIFF) na mrembo Wema Sepetu kuibuka mshindi kwa upande wa waigizaji wa kike, msanii mkongwe nchini Amri Athumani ‘Mzee Majuto’ amesema mrembo huyo hawezi kuwa mkali kushinda Riyama Ally.

    Katika kipengele hicho Wema alikuwa akichuana na wasanii nane na filamu walizoigiza kwenye mabano akiwemo Getrude Mwita (Bantu), Rachel Kayuga (Safari ya Gwalu), Aisha Mwajumla (Watatu), Riyama Ali (Mama wa Marehemu).

    Wengine ni Amina Rashid (Bandidu), Hawa Abeid (Genge), Sharifa Mansury (Kivuli cha ahadi) na Neema Mangowi (Malaika) wakati Wema yeye aliingia kupitia filamu yake ya Heven Sent.

    Akizungumza na MCL Digital leo Aprili 4, Mzee Majuto amesema kwake bado Riyama ni mkali na hawezi kufananishwa na Wema katika kuuvaa uhusika anapokuwa mbele ya kamera.

    “Mimi nimekaa kwenye fani hii ya uigizaji siku nyingi, najua nani mwigizaji nani amevamia fani japo najua kuna watu wataniponda, lakini ukweli Riyama alistahili kubeba tuzo ile na sio Wema,” amesema msanii huyo anayewavunja watu mbavu kwa vichekesho.

    Pia ametaja sababu ambazo ameona ndizo zilizomwezesha Wema kushinda kuwa zimetokana na mambo ya kidijitali, kwa yeye kuwa na mashabiki wengi mtandaoni ambao waliweza kumpigia kura tofauti na wasanii wengine alioshindanishwa nao.

    Katika ushauri wake, Mzee Majuto amesema ni vizuri wakati mwingine majaji wasiangalie hilo la upigaji kura na badala yake waangalie vipaji vya watu kwani kwa kufanya hivyo itawavunja moyo wengine wanaotaka kufanya vizuri kwa kuona tayari wana washindi wao mfukoni.

    Hata hivyo kwa upande wa msanii bora wa kiume, Mzee Majuto amesema Ahmed Salim ’Gabo’ amestahili kwa kuwa hakuna asiyejua kipaji cha msanii huyo tangu alivyoanza kung’ara kwenye filamu mbalimbali alizoigiza.

    Katika tuzo hizo, vipengele 19 vilikuwa vikishindaniwa, ambapo kwa washindi bora wa kike na kiume kila mmoja aliondoka na tuzo na Sh5 milioni taslimu, wakati vipengele vingine walipata Sh1 milioni.

    Unafikiri mzee majuto yuko sahihi?
    celine dion
    celine dion
    Junior Member


    MZEE MAJUTO  ANASEMA WEMA SEPETU AWEZI KUWA MKALI KUSHINDA RIHAMA JE NI KWELI? Empty Re: MZEE MAJUTO ANASEMA WEMA SEPETU AWEZI KUWA MKALI KUSHINDA RIHAMA JE NI KWELI?

    Post by celine dion Wed Apr 11, 2018 10:14 am

    ni kweli
    Anonymous
    selunkuma
    Guest


    MZEE MAJUTO  ANASEMA WEMA SEPETU AWEZI KUWA MKALI KUSHINDA RIHAMA JE NI KWELI? Empty Re: MZEE MAJUTO ANASEMA WEMA SEPETU AWEZI KUWA MKALI KUSHINDA RIHAMA JE NI KWELI?

    Post by selunkuma Thu Apr 12, 2018 11:50 am

    hata mimi nilishangaa
    James Kub
    James Kub
    Junior Member


    MZEE MAJUTO  ANASEMA WEMA SEPETU AWEZI KUWA MKALI KUSHINDA RIHAMA JE NI KWELI? Empty Re: MZEE MAJUTO ANASEMA WEMA SEPETU AWEZI KUWA MKALI KUSHINDA RIHAMA JE NI KWELI?

    Post by James Kub Thu Apr 12, 2018 5:54 pm

    yuko sawa mzee
    Roy
    Roy
    Founder


    MZEE MAJUTO  ANASEMA WEMA SEPETU AWEZI KUWA MKALI KUSHINDA RIHAMA JE NI KWELI? Empty Re: MZEE MAJUTO ANASEMA WEMA SEPETU AWEZI KUWA MKALI KUSHINDA RIHAMA JE NI KWELI?

    Post by Roy Sun Apr 15, 2018 5:56 pm

    na huo ndio ukweli

    Sponsored content


    MZEE MAJUTO  ANASEMA WEMA SEPETU AWEZI KUWA MKALI KUSHINDA RIHAMA JE NI KWELI? Empty Re: MZEE MAJUTO ANASEMA WEMA SEPETU AWEZI KUWA MKALI KUSHINDA RIHAMA JE NI KWELI?

    Post by Sponsored content


      Current date/time is Fri May 10, 2024 5:15 pm