Shirikisho la soka barani Ulaya(UEFA) limethibitisha kwamba timu za soka zinaweza kuweka majina 12 ya wachezaji wa ziada kwenye mechi za fainali za Ligi ya Mabigwa(UEFA Champions), Ligi ya EUROPA na Super Cup. Kwa sasa idadi hiyo ni wachezaji 7
Aidha, katika sheria hiyo mpya ambayo itaanza kutumia msimu ujao wa soka, timu zitaweza kufanya mabadiliko mara nne katika hatua ya mtoano ya michuano, huku badiliko hilo la nne likiruhusiwa wakati wa dakika za nyongeza
Timu zitaruhusiwa kusajili wachezaji wapya watatu kwenye michuano hiyo baada ya hatua ya makundi kumalizika. Ikimaanisha mchezaji anaweza kuchezea timu moja wakati wa hatua ya makundi halafu akasajili na timu nyingine(kwenye dirisha la usajili) na timu hiyo kumsajili UEFA kucheza katika hatua ya mtoano
Pia katika UEFA mechi zake zote zitakuwa zinachezwa muda wa 8pm GMT (kwa Tanzania: saa 4:00 usiku majira ya joto, saa 5:00 usiku majira ya baridi)
Katika michuano ya michuano ya EUROPA hatua ya makundi mpaka 16 bora mechi zitakuwa zinaanza saa 5:55pm GMT na 8pm GMT(Kwa Tanzania; 1:55 usiku na 4:00 usiku majira ya joto, 2:55 na 5:00 majira ya baridi). Michezo ya robo, nusu na fainali itachezwa saa 8pm GMT (kwa Tanzania: saa 4:00 usiku majira ya joto, saa 5:00 usiku majira ya baridi)
Aidha, katika sheria hiyo mpya ambayo itaanza kutumia msimu ujao wa soka, timu zitaweza kufanya mabadiliko mara nne katika hatua ya mtoano ya michuano, huku badiliko hilo la nne likiruhusiwa wakati wa dakika za nyongeza
Timu zitaruhusiwa kusajili wachezaji wapya watatu kwenye michuano hiyo baada ya hatua ya makundi kumalizika. Ikimaanisha mchezaji anaweza kuchezea timu moja wakati wa hatua ya makundi halafu akasajili na timu nyingine(kwenye dirisha la usajili) na timu hiyo kumsajili UEFA kucheza katika hatua ya mtoano
Pia katika UEFA mechi zake zote zitakuwa zinachezwa muda wa 8pm GMT (kwa Tanzania: saa 4:00 usiku majira ya joto, saa 5:00 usiku majira ya baridi)
Katika michuano ya michuano ya EUROPA hatua ya makundi mpaka 16 bora mechi zitakuwa zinaanza saa 5:55pm GMT na 8pm GMT(Kwa Tanzania; 1:55 usiku na 4:00 usiku majira ya joto, 2:55 na 5:00 majira ya baridi). Michezo ya robo, nusu na fainali itachezwa saa 8pm GMT (kwa Tanzania: saa 4:00 usiku majira ya joto, saa 5:00 usiku majira ya baridi)